Benki ya NMB imetoa msaada wa vifaa vya hospitali kwaajili ya zahanati ya chuo kikuu cha Dodoma vyenye thamani ya Shilingi milioni 20.

 

 Vifaa hivyo vilivyotolewa kwa Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Dodoma – Prof Shaaban Mlacha ni pamoja na - Jokofu kwaajili ya benki ya Damu, Meza ya upasuaji (Operating Table), Taa maalumu za kwenye chumba cha upasuaji (Overhead Operating Lamp) vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 20.

 

 Msaada huo ulipokelewa vyema na uongozi wa chuo kikuu cha Dodoma kusifu juhudi za benki ya NMB katika kuchangia maendeleo nchini.