1. Zoezi hili litaendeshwa na NMB kwenye kurasa zao za Facebook, Instagram, Twitter na kwenye tovuti. Shule/ hospitali zitakazohitimu zitakabidhiwa vifaa kama vitanda vya wagonjwa, vitanda vya kujingulia au vifaa vya kuezeka kulingana na taratibu zetu za huduma kwa jamii.

Washiriki wanakubaliana na miongozo ifuatayo:

  1. Kushiriki kwenye shindano hili, mshiriki anatakiwa kuwa na umri wa miaka 18 na kuendelea.
  2. Mshiriki atatakiwa kuchagua shule/ hospitali iliyo karibu naye yenye uhitaji wa vifaa vya kuezeka au vitanda vya wagonjwa na vya kujifungulia (atatakiwa kuambatisha picha ya uthibitisho wa mahali alipo).
  3. Shule/ hospitali itakayochaguliwa ni sharti iwe ya umma (ambatanisha mawasiliano ya shule/ hospitali).
  4. Mshiriki atatakiwa kupakua ‘template’ kutoka kwenye tovuti yetu https://www.nmbbank.co.tz/csr kisha kujaza fomu na kuwasilisha kwenye This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. pamoja na taarifa zao kamili za mawasiliano.
  5. Maombi yote yatathaminishwa kupitia matawi yetu ya NMB kulingana na mahali yalipotolewa.
  6. Shule/ hospitali inatakiwa kuwa inafanya kazi kwa muda mrefu na siyo iliyoanzishwa hivi karibuni.
  7. Mshiriki atatakiwa kutu’like’ na kutufuata kwenye mojawapo ya kurasa zetu za Facebook, Twitter na Instagram.
  8. NMB inayo haki ya kumbatilisha mshiriki (na kumchagua mshiriki mwingine) kama wanayo sababu kwamba hajakidhi vigezo au amekwenda kinyume na miongozo.
  9. Baada ya vifaa kuwa tayari, mshiriki atapewa taarifa ya hatua za makabidhiano.
  10. Endapo kutatokea kutoelewana kuhusu hatua, utendaji, matokeo na masuala yote kuhusu shindano hili, NMB (au wakala wake aliyeidhinishwa) watakuwa na maamuzi ya mwisho.