SWL ni mkopo usiohitaji dhamana unaotolewa kwa watumishi wa Serikali; wa kudumu/mkataba na wafanyakazi wa sekta binafsi. Benki haimlazimishi mteja kuwa na dhamana ya aina yoyote isipokuwa atatakiwa kupitishia mshahara wake Benki ya NMB baada ya benki kuingia mkataba na mwajiri wake.

Sifa

  • Unaweza kupata mkopo mpaka wa Sh50 milioni
  • Unaweza kuchukua mkopo mwingine juu ya ule wa awali muda wowote
  • Riba nafuu hutozwa kadri mkopo unavyopungua
  • Muda wa marejesho ni kati ya mwaka mmoja mpaka miaka sita
  • Mkopo unakatiwa bima dhidi ya kifo au ulemavu wa kudumu

Unachohitaji ili kupata Salaried Workers Loan

  • Pitishia mshahara wake Benki ya NMB
  • Mwajiri wako kuwa na mkataba na Benki ya NMB
  • Nakala 3 za taarifa za mshahara
  • Barua ya ajira/mkataba
  • Kitambulisho cha kazi
  • Mteja atatakiwa kusaini fomu ya kuomba mkopo
  • Awe mfanyakazi mwenyewe

Faida za NMB Salaried Workers Loan

  • Tunanunua mikopo ya taasisi nyingine za fedha au Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB)
  • Hakuna masharti ya matumizi ya fedha za mkopo husika
  • Unaweza kuutumia mkopo huo kama mtaji wa kuanzisha biashara
  • Uhakika na uwezo wa kukamilisha mahitaji yako
  • Mkopo unakatiwa bima dhidi ya kifo au ulemavu wa kudumu
  • Hakuna adhabu au makato yasiyo ya msingi
  • Uhakika wa muda na utaratibu wa marejesho kama ilivyoainishwa kwenye mkataba
  • Unaweza kuchukua mkopo mwingine juu ya ule wa awali
  • Marejesho ya kila mwezi hayaongezeki hata kama mshahara wako ukipanda.

Kwa msaada zaidi, tafadhali tembelea tawi la Benki ya NMB lililo jirani yako au tupigie bure kwa namba ya huduma kwa wateja – 0800 002 002